Wenyeji wa mashindano hayo huko Gold Coast - Australia wanaongoza na dhahabu 39, Uganda ikiwa katika nafasi ya 12, Kenya ya 21 na Mauritius ya 23.
![]() |
| Timu ya Rwanda ya voliboli ya ufukweni jana imeshinda mechi yake ya kwanza dhidi ya Singapore |
![]() |
| Fathiya Pazi amemshinda mpinzani wake wa Tuvalu 4-0 na hivyo kuwa mchezaji pekee wa Afrika Mashariki kuibuka mshindi mechi za tenisi ya meza kufikia sasa |
![]() |
| Akishinda mechi yake ya pili leo jioni ya tenisi ya mezani, Fathiya Pazi ataingia awamu ya mtoano. |
![]() |
| Bondia wa Uganda Juma Miiro amemshinda Shafi Bakari wa Kenya uzani wa light-fly na kufuzu nusu-fainali hivyo basi kuihakikishia Uganda medali ulingoni |
![]() |
| Shafi Bakari wa Kenya aliibusu sakafu raundi ya pili na kuhesabiwa hadi nane. Matumaini ya Kenya sasa yako kwa Christine Ongare uzani wa fly anayecheza kesho na bondia wa Sri Lanka |
![]() |
| Masoud Mtalaso wa Tanzania (kushoto) na Halima Nambozo wa Uganda wote wamepoteza mechi zao za kwanza katika mchezo wa tenisi ya mezani. |






Comments
Post a Comment