Translate

Kimbunga Irma chavamia Marekani

Kimbunga Irma kimepiga jimbo la Florida nchini Marekamani, ambapo  awali  kilikikumba  kisiwa cha Marco magharibi mwa pwani mwa Florida, kikiwa na upepo wa kasi ya kilomita 192 kwa saa lakini kwa sasa kimeshuka kutoka kiwango cha tatu hadi cha pili.
Gari ikiwa imeangushwa na mafuriko katika mtaa wa  Miami


Zaidi ya nyumba milioni 3.4 katika jimbo la Florida zimekosa nishati ya  za umeme huku sehemu za mji wa Miami zikifurika maji.

Vifo vitatu vinavyotokana na kimbunga hicho vimeripotiwa wakati kimbunga hicho kikielekea sehemu za Kaskazini

Kituo kinacho husika na vimbunga nnchini  Marekani kinasema kimbunga hicho kimesababisha upepo sehemu tofauti za katikati mwa Florida.

Mapema kimbunga hicho kilipiga maeneo yanayozunguka mji wa Fort Myers, huku kikiharibu maeneo ya Caribbean na kuuwa takribani watu 28. 

Kutokana na hali hiyo takribani watu milioni 6.3 huko Florida wameambiwa wahame.

Comments